Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2017

USIMUOGOPE MFALME WA ASHURU.

             Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu .         Karibu tujifunze Neno la MUNGU.    MUNGU akupe Neema juu ya ujumbe huu, ukaone Neema ya kutokea Ukaone nguvu ya MUNGU ikiambatana na wewe kupitia Neno lake. Kumbuka Biblia inasema katika Zaburi 107:20 kwamba " Hulituma neno lake, huwaponya , Huwatoa katika maangamizo yao ."      Kwa hiyo Neno la MUNGU ambalo MUNGU huwa analiachilia, analituma lije kwako wakati mwingine lina kazi nyingi.         Kazi mojawapo ya Neno hilo ni kuponya, kazi mojawapo ni kukuondoa kwenye maangamizo , kazi nyingine ni kukuimalisha , lina kazi nyingi Neno la MUNGU , ni zaidi ya kazi kumi Neno la MUNGU linaweza likafanya katika maisha yako . Ujumbe wa Leo ni Neno limetumwa kwako ili kukuambia kwamba usimwogope Mfalme wa Ashuru .       ...

NI SOSPETER KORONGO + NAOMI MNUA WAANZA KAMPENI

Picha
  FOLENI KAMA KAWAIDA INATEMBEA         Hongera sana kijana wetu, mtoto wetu wa nyumbani SOSPETER KORONGO na binti yetu NAOMI kwa uamuzi wenu wa baraka na wa kuigwa na kila kijana.          'FOLENI INAZIDI KUTEMBEA' Hii ndiyo kauli ambayo kila kijana ukikutana naye utasikia akiitamka, hususani wale vijana ambao bado hawajaoa na kuolewa, ukiwauliza wataoa au kuolewa lini utawasikia wakikujibu hivyo kuwa 'FOLENI INATEMBEA-  Yaani bado naye yuko kwenye msafara, at any time atafikiwa zamu yake.          Vijana waliotangaza uchumba wakipongezwa na vijana wenzao muda mchache baada ya kuvishana PETE YA UCHUMBA kanisani katika ibada.     Sehemu ya waumini wa kanisa hilo katika ibada wakisimama kuwaombea vijana hao waliokuwa madhabahuni muda mchache baada ya kutangaza uchumba. [Picha na Ev. Elimeleck Ndashikiwe] Ashukuriwe Mungu wa mbinguni kwa fadhili zake nyi...

SHEREHE YA WATOTO KANISANI

Picha
SHEREHE YA WATOTO WA HEMA YA SIFA KANISANI KATIKA PICHA              Shalom Shalom mtu wa Mungu upendwaye sana                         Hakika tar 13/08/2017 ilikuwa ni siku ya pekee sana kwa watoto wa kanisa la Pentekoste Hema ya Sifa TEGETA KIBAONI, Hakika watoto walipendeza sana tena sana kuliko Watoto wa HEMA YA SIFA wakihudumu katika ibada,  iliyoambatana na sherehe yao.       Kikundi cha kusifu na kuabudu kikiwa katika madhabahu kikihudumu katika ibada iliyoambatana na sherehe ya watoto    [Picha na Ev. Elimeleck Ndashikiwe]   Sehemu ya waumini waliofurika katika ibada kuungana na watoto wao pamoja kusherehekea sikukuu ya watoto wao. Watoto wakiwa wametulia pamoja wakisubiri maelekezo kutoka kwa mwalimu wao wajue nini kinac...

USIING'ANG'ANI DHAMBI KAMA UGALI WA DONA

                 Na Mwl Pastor Boniphace Mbise  BWANA YESU atukuzwe mpendwa wangu .     Karibu tujifunze Neno la MUNGU la uzima.                Leo nazungumzia M adhara ya dhambi katika maisha ya Mtu ,       lakini mwanzo kabisa naomba kila mtu ajue kwamba madhara mabaya zaidi ya dhambi ni ziwa la moto,     ndio maana MUNGU kila Leo anawaonya wanadamu ili waache dhambi , MUNGU anasema :              '' Tazama, roho zote ni mali yangu; kama vile roho ya baba ni mali yangu , ndivyo ilivyo roho ya mwana mali yangu ; roho ile itendayo dhambi itakufa . Ezekieli 18:4 ''       Madhara mengine ya dhambi ni kifo cha mapema.      ...