KITABU CHA YOHANA MTAKATIFU



Bwana Yesu asifiwe sana wapendwa,

Mistari muhimu: "Hapo mwanzo kulikuwako na Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu ... Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli "(Yohana 1: 1,14).

"Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, 'Tazama mwana kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!" (Yohana 1:29).


Ev. Elimeleck Ndashikiwe 

"Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe Pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele" (Yohana 3:16).

"Yesu akajibu, akawaambia, 'Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwaamini yeye aliyetumwa na yeye" (Yohana 6:29).

"Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu. Mimi nilikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele" (Yohana 10:10).

"Nami nawapa uzima wa milele, wala hawatapotea kamwe, wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu" (Yohana 10:28).

"Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unayasadiki hayo?" (Yohana 11: 25-26).

"Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi" (Yohana 13:35).

"Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi" (Yohana 14: 6).

"Yesu akamwambia, mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba'" (Yohana 14: 9).

"Uwatakase kwa ile kweli. Neno lako ndiyo kweli" (Yohana 17:17).

"Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha! Akainama kichwa, akaisalimu roho yake "(Yohana 19:30).

"Yesu akamwambia, wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki." (Yohana 20:29).

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUPIGA HATUA KUBWA ZAIDI KIROHO

WATUMISHI WA MUNGU TUSIDHARAULIANE

JE, UNAIJUA KARAMA YAKO? By Ev. Elimeleck S Ndashikiwe