Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2017

ANAYESTAHILI KUABUDU NI YUPI?

MH:    EV. SAMSON JOHN SOMO:   KUABUDU              Kuabudu maana yake ni kitendo cha kumkaribia MUNGU au chochote kile kwa kukitukuza katika madhabahu ya aina yoyoyte ile.             Kwa maana nyingine twaweza kusema kuwa,kuabudu ni kufanya tendo la kifalme ktk madhabahu na kutoa dhabihu kimiungu.      ISAY 43:7 `Kila mmoja aliyeitwa kwa jina langu, niliyemuumba kwa ajili ya utukufu wangu., mimi nimemumba, naam, mimi mnimemfanya.                 Hapa tunaona namna ambavyo MUNGU mwenyewe anajitambulisha kwa watu wote kuwa yeye ndiye alliyewafanya na kuwaumba.          Hivyo basi, kwa sababu hiyo, Kila yeyote aliyeumbwa na kufanywa na MUNGU, anatakiwa kujua ni wapi anastahili kuelekeza ibada yake.     ...

BIBLE STUDY 8th DAY

Picha
PRE: BABU  &  BIBI SOMO: KITABU CHA MATENDO YA MITUME SURA YA SITA    {MDO 6}                       Bwana Yesu Asifiwe ndugu yangu mpendwa,  unayeusoma ujumbe huu ikiwa ni mwendelezo wa masomo yanayoendelea hapa kanisani na walimu wetu'.           Matendo 6:1 ...................... Hata siku zikle wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung`unikoo ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku.           Katika kitabu hiki cha Matendo ya Mitume tunakutana na mambo kadha wa kadha ambayo yanatupatia ujumbe kamili kuhusiana na kile ambacho Mtumishi wa Mungu Paulo alichokuwa akikimaanisha na kukielezea. MAMBO MUHIMU 1. Makuhani waliitii Injili 2, Wajane walisahauliwa 3. Walinung`unika ...

BIBLE STUDY

Picha
MHU: BABU  AND  BIBI SOMO: MUHTASARI AU MAREJEO KITABU CHA WAGALATIA Bwana Yesu basifiwe ndugu yangu Mpendwa,                  Baada ya kuwa tumefikia mwisho wa kujifunza kitabu hiki cha Wagalatia sura zake zote sita, walimu wetu waliweza kujiridhishakama wanafunzi tumefaidika na tumeelewa ninikatika KITABU HIKI CHA wagalatia. Ongeza kichwa MASWALI YA CHANGAMOTO 1. Nini hasa kilichokugusa katika kitabu hiki cha Wagalatia? 2. Kitabu cha Wagalatia kimewezaje kuyabadilisha maisha yako? 3. Utafanya nini ili usababishe mabadiliko katika maisha yako?                        Kila mmoja wetu mwanafunzi darasani aliweza kutafakari ni namna gani alivyoweza kukielewa kitabu hiki cha WAGALATIA chenye sura sita tu.      Ni kweli,  kuna mambo mengi sana ambayo yamea...

BIBLE STUDY 6Th DAY

Picha
SEMINA YA WANACHUO CHA BIBLIA MH:  BABU  NA  BIBI SOMO: WAGALATIA SURA YA NNE    {URITHI, UHURU NA UTUMWA}                                 Bwana Yesu asifiwe ndugu yangu mpendwa, natumai ya kuwa u mzima wa afya tele na Neema ya Mungu inatembea upande wako.            Ni wakati mwingine tena nikufikishie ujumbe huu ambao tunaendelea nao hapa kanisani tukiwa na walimu wetu hawa {BABU NA BIBI}.           Leo tulijifunza kitabu cha Wagalatia sura ya Nne. Kuna mambo mengi sana tumeyaona hapa na kujaribu kujifunza na kukumbushwa mambo kadhaa juu ya safari yetu hii tuliyonayo ya kwenda Mbinguni.   WAGALATIA 4;1........ Lakini nasema ya kuwa mrithi wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa...

JE, UNAIJUA KARAMA YAKO? By Ev. Elimeleck S Ndashikiwe

Bwana Yesu Asifiwe Watumishi wa Mungu.             Je unakitumia kipawa chako katika kusudi la MUNGU?       Kila mmoja wetu kuna kusudi la MUNGU kuwepo kwaka Wokovu wa Bwana YESU . Kila mmoja kuna hatima njema ya MUNGU aliyomkusudia kama akimtii MUNGU . Hakuna aliyezaliwa kwa bahati mbaya .             Hakuna mtu aliyezaliwa kwa matakwa tu ya mwanaume na mwanamke. Karama ni nini ?       Kipawa anachokuwa nacho mtu kwa sababu ya kumwabudu sana MUNGU .        Kipawa ni uwezo mtu aliozaliwa nao ambao humwezesha kufanya jambo Fulani vizuri .           Kwa sababu kuna kuzaliwa upya kiroho baada ya kuokoka basi kuna vipawa pia huzaliwa baada ya sisi kumpokea Bwana YESU na ROHO MTAKATIFU kuingia ndani mwetu, maana ROHO ndiye ...

BIBLE STUDY 4th DAY

Picha
MH; BABU  &  BIBI SOMO: UCHAMBUZ WAKOLOSAI SURA YA NNE {KOL 4:1-18}                              LEO TUNAENDELEA NA SURA YA NNE YA KITABU CHA WAKOLOSAI MST 1-2 "Ninyi akina bwana wapeni watumwa wenu yaliyo haki na ya adili,  mkijua ya kuwa ninyi nanyi mna Bwana Mbinguni. 2. Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukurani.        Mtume Paulo alikuwa akiongea na watu wale ambao wanaishi na watumishi majumbani mwao {wafanya kazi}, akichukulia mfano wa utumishi katika nyumba ya Bwana, Akiwakumbusha namna wanavyoweza kuishi nao kwa uzuri sawa na vile wao walivyo chini ya Bwana mwingine ambaye ni Mungu wa Mbinguni.    Lakini pia akiwakumbusha kuwapongeza pale wanapokuwa wametenda vema na kuwafundisha yaliyo ya adili, yaani wajiheshimu na kuepukana na kila namna ya ubaya.       ...

NGUVU YA HASIRA

Picha
SEHEMU YA PILI UCHAMBUZI     Mwalimu: BABU  NA  BIBI                       KITABU: WAKOLOSAI 3:8.... .............                                   Bwana Yesu asifiwe Mtumishi wa Bwana,  unayesoma ujumbe huun na unayeendelea kufuatana nasi katika mfululizo wa masomo yetu yanayoendelea hapa jijini Dar Es Salaam,  katika kanisa la PENTECOST TEBARNACLE OF PRAISE,  TEGETA KIBAONI. Sasa tuendelee....................                                       Katika kitabu hiki cha wakolosai sura ya 3 inatupa nuru na mwanga wa kutosha kabisa kuweza ...

BIBLE STUDY

MH; BABU  &  BIBI SOMO;  SURA YA PILI YA KITABU CHA WAKOLOSAI                                  Mtumishi wa Mungu PAULO aliiandika hii sura kwa ajili ya watu wa MUNGU, ambao tayari wamekuwa wafuasi wa Mungu kwelikweli kwa njia ya YESU KRISTO.                        Amejaribu kulikumbusha kanisa kwa habari ya kujitambua na kujua wito wao mkuu, akiwasihi kuishi wakiifuata njia ile iwapasayo kuiendea ambayo walihubiriwa kwa hapo mkwanza na Yesu mwenyewe,                           Zaidi sana akiwasihi kuyatafakari yale yaliyo juu zaidi kule Yesu aliko  {mstari 1}, anasema,...

WATUMISHI WA MUNGU TUSIDHARAULIANE

     Bwana YESU atukuzwe ndugu yangu ! Karibu tujifunze Neno muhimu sana.          Njia mojawapo ya kukufanya uwe mtumishi mzuri wa MUNGU ni wewe kumtumikia Bwana YESU kwa moyo wa upendo huku ukiwahesabu watumishi wenzako kuwa ni bora kuliko nafsi yako .              ''Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.            Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.      Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; Wafilipi 2:3-5''          Kuwaona watumishi wenzako ni bora kuliko wewe itakusaidia ili usiwe na kiburi na utakuwa unatimiza kusudi la ...